WASHINDI WA WIKI YA
UTUMISHI WA UMMA 2014
Tarehe 23 Juni kila mwaka ni siku maalum ya
Watumishi wa Umma. Nchi wanachama wa Umoja wa Afrika (AU) huadhimisha siku hiyo kwa pamoja kwa lengo la kutambua
mchango wa Watumishi wa Umma katika maendeleo ya Nchi zao. Kaulimbiu kwa mwaka
2014 ni “Mkataba wa Misingi na Kanuni za
Utumishi wa Umma Barani Afrika ni Chachu ya Kuimarisha Utawala Bora na
Uendeshaji wa Shughuli za Serikali kwa Uwazi”
Hapa nchini Maadhimisho haya huratibiwa na
Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma. Mwaka 2014 Taasisi za Umma 88
zilishiriki na kushindanishwa katika maeneo mbalimbali ya utoaji huduma.
Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Y. Sefue
alikabidhi zawadi kwa Taasisi zifuatazo zilizofanya vyema zaidi kwa kushiriki
katika Maonesho yaliyofanyika katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es
salaam.
1.
BANDA BORA
(I)
Mfuko
wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF).
(II)
Mamlaka
ya Chakula na Dawa Tanzania (TFDA).
(III)
Wizara
ya Maji.
2.
MAPAMBANO DHIDI YA UKIMWI MAHALI PA
KAZI
(I)
Wizara
ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa.
(II)
Ofisi
ya Rais, Tume ya Utumishi wa Umma.
(III)
Mamlaka
ya Viwanja vya Ndege Tanzania.
3.
UBUNIFU KATIKA KUBORESHA UTOAJI
HUDUMA
(I)
Wizara ya Maji – washindi kupitia Teknolojia ya
kupunguza madini ya floride katika maji kwa kutumia mifupa ya ng’ombe.
(II)
Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO)-washindi wa pili kupitia kifaa
kiitwacho Umeme tayari “ready Board”
kinachowezesha wananchi kupata umeme bila kusuka na kusambaza nyaya za umeme
(wiring) katika nyumba.
(III)
Wakala ya Vipimo (WMA)-washindi wa tatu kupitia mfumo wa
kieletroniki “Clock in and clock out task
information system” unaotumika kudhibiti muda wa kuingia na kutoka kazini.
hongera sana kwa washindi!!!!
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni